PATA MATUKIO MBALI MBALI YA KIJAMII POPOTE ULIPO!

Sunday, October 24, 2010

MSALABA MWEKUNDU KUTOA HUDUMA YA KWANZA SIKU YA UCHAGUZI


                  ...Baadhi ya kazi wanazofanya msalaba Mwekundu nchini...
       Watendaji wa Shirika la Msalaba Mwekundu wakimwahisha hospitalini mmoja wa waathirika wa mabomu 11 yaliyolipuliwa jana katika
Watendaji wa Shirika la Msalaba Mwekundu wakimwahisha hospitalini mmoja wa waathirika wa mabomu 11 yaliyolipuliwa  Juni 6 2009, katika kambi ya Jeshi la Ulinzi wa Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Mbagala. 


CHAMA cha Msalaba Mwekundu nchini kupitia kikosi chake maalumu cha Uokoaji na Maafa Mkoa wa Dar es Salaam (Action Team) kimejipanga kuhakikisha kinatoa huduma ya kwanza na dharura kwa kiwango cha juu siku ya uchaguzi.
Mwenyekiti wa Chama cha Msalaba Mwekundu Mkoa wa Dar es Salaam, Mayasa Mikidadi, alieleza hayo jana jijini Dra es Salaam muda mfupi baada ya kumalizika kwa uchaguzi wa viongozi wapya wa kikosi hicho.
Alisema chama hicho imejiandaa vya kutosha kutoa huduma ya kwanza na ya dharura siku ya kupiga kura na matatizo yote ya dharura.
“Ni hakika kazi iliyopo mbele yetu ni ngumu, lakini hakika uwezo tunao na tutaifanya kwa nguvu zote ili kuhakikisha kila Mtanzania anapata haki ya kupiga kura kwa usalama,” alisema Mayasa.
Aliendelea kusema kikosi hicho kitafanya shughuli za uokoji siku hiyo ambazo zitawalenga watu watakao kuwa wamezidiwa katika foleni, wagonjwa pamoja na kuwasaidia walemavu wa aina yote kusaidiwa kwa lolote litakalotokea wakati wa upigaji wa kura hizo.
Aidha, katika uchaguzi huo, viongozi  waliokuwapo kwa muda wa miaka kadhaa walijiuzulu na kupisha uongozi mpya, ambao ulifanywa kwa njia ya amani, huku wakichaguana kwa kanuni ya kupiga kura.
Viongozi waliochaguliwa katika uchaguzi huo ni pamoja na Dk. Suphian Juma (Kamanda Mkuu), Feruzi Mpili (Kamanda Msaidizi), huku nafasi ya katibu ikichukuliwa na Amina Mwalimu.
Uongozi huo mpya ulishukuru kwa kuchaguliwa kwao kutokana na kuwa na imani nao huku kuahidi kushirikiana bega kwa bega na wanachama wa matawi yote mkoani hapo.
Kwa upande wake Kamanda mpya, Dk. Suphian, aliwashukuru wanachama wote kwa kumchagua huku akiwataka kila mwanachama kushirikiana bega kwa bega ili kufanikisha uongozi makini.

Katika uongozi huo, pia ulisimamiwa na Mratibu wa Mkoa wa chama hicho, Grace Mawala pamoja na  Mwekiti wa Wilaya,Dr Mambo
....Kikosi hicho maalum kinafanya shughuli mbalimbali za kujitolea zikiwemo za majanga na maafa, ususani ya dharura kama ya mabomu ya Mbagala pamoja na maafa ya Same na kilosa, ikiwemo kufunga mahema,kusimamia huduma ya kwanza na maswala yote ya kitaalm ya uokoaji.. 


No comments:

Post a Comment