PATA MATUKIO MBALI MBALI YA KIJAMII POPOTE ULIPO!

Tuesday, October 19, 2010

CHADEMA,CCM WAENDELEA NA KAMPENI ZAO MIKOANI LEO!!

Matukio ya kampeni kwa wagombea wa Urais wa Chadema na CCM, katika mikoa mbalimbali nchini Tanzania leo .....CHADEMA HOOOOYEEEEEEEE! SINGIDA MJINI!

Slaa kupokelewa Singida;
Wananchi wa mji wa Singida na vitongoji vyake, wakimlaki mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Slaa, mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa kituo cha mabasi cha zamani mjini humo, ambako alihutubia mkutano wa kampeni mapema leo.
Kushangilia ujio wa Slaa;
Baadhi ya wakazi wa mji wa Singida, wakishangilia mara baada ya kuwasili kwa mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, katika Uwanja wa Kituo cha Mabasi cha zamani.
Maendeleo (CHADEMA), Josephat Isango, akwahutubia wananchi wa mji huo na vitongoji vyake, katika mkutano wa kampeni wa mgombea urais kwa tiketi ya chama hicho, Dk. Willibrod Slaa,
Kumsikiliza Slaa;
Baadhi wa wakazi wa kiji cha Ikungi katika jimbo la Singida Mashariki, wakimsikiliza kwa makini mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, katika mkutano wa kampeni kijijini hapo 

Slaa kuhutubia 
Mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, akiwahutubia wananchi wa mji wa Singida, katika mkutano wake wa kampeni kwenye Uwanja wa Kituo cha Mabasi cha zamani mapema jioni ya leo. (Picha zote kwa Hisani ya  Joseph Senga-Singida)

Mkutano wa Mgombea Urais wa CCM, Jakaya Kikwete, Mkoani Lindi katika  mji wa Ruangwa leo; 
 CCM NGUVU ZAIDI KASI ZAIDI .USHINDI RAZIMA 2010!!
Wananchi wa Ruangwa wakisalimiana na  Mgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi Mheshimiwa Jakaya Kikwete  muda mfupi kabla ya mkutano wa kampeni mchana wa leo.
                        Rais Jakaya Kikwete ambaye pia ni mgombea wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi akimsikiliza Bi Rehema Omar Mitacha mkazi wa mtaa wa Nachingwea katika mji wa Ruangwa ambaye ni mlemavu wa miguu muda mfupi kabla ya kuhutubia mkutano wa kampeni tarehe 
Umati mkubwa ukimlaki Rais Jakaya Kikwete katika kampeni hiyo Rungwe..
                        Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ambaye ni Mgombea Urais kupia CCM akihutubia wananchi wa mji wa Ruangwa, mkoani Lindi kwenye mkutano wa kampeni mapema leo (Picha zote kwa msaada wa   John Lukuwi)...

Angalizo; Chondechonde viongozi wetu tukumbuke sera na ahadi makini zitakazomkomboa mtoto sambamba na haki zake.

Pia tunaomba muendelee kututumia picha za kampeni kila siku sambamba na matukio mbalimbali yanayoendelea nchini; Email; nimkalameck@yahoo.com


 






No comments:

Post a Comment