PATA MATUKIO MBALI MBALI YA KIJAMII POPOTE ULIPO!

Monday, October 18, 2010

MATOKEO YA KURA ZA JAMII;SHY-ROSE APATA 89%,KIKWETE 85%

Shyrose Bhanji  amepata asilimia 89,Rais Jakaya Kikwete asilimia 85, Reginald Mengi 83 katika maswala mbalimbali ya kijamii ikiwemo ukaribu kwa watoto na makundi ya rika zote.


Alama hizi zimeweza kupigwa na wananchi zaidi ya 254 kutoka karibu nchi 23 Duniani kote, wananchi wengi walipiga kwa kuangalia matukio kadhaa yawaliyofanya watu hawa ambapo tulitoa angalizo ikiwemo kwa wananchi kupendekeza hilo.


Wengi wa wananchi hao waliweza kufuatilia kupitia mitandao na taarifa kadhaa za Watu hawa, mitandao hiyo ni pamoja na (Facebook,Blogs,Magazeti na Televisheni,redio) ambapo waliweza kutuma 'sms' katika namba +255719076376 na katika email; nimkalameck@yahoo.com/ sambamba na katika komenti za mtandao huu.


Awali majina kadhaa waliyapitisha yakiwemo ya Rais Jakaya Kikwete, Shy-Rose Bhanji(Mwanaharakati), Reginald Mengi(Mfanyabiashara), Mizengo Pinda(Waziri Mkuu),Dr Charles Kimei (CRDB), Mama Salma Kikwete (First Lady).


Alama walizotoa wadau hao ni pamoja na matukio waliyofanya katika shughuli mbalimbali za kijamii nchini pamoja na ukaribu wao kwa watoto.


Zifuatazo ni kati ya mambo ambayo yameweza kumpa kura Shy-Rose Banji kupata asilimia hizo 89.

Shy-Rose akiwa na baadhi ya wanafunzi wa shule moja nchini Tanzania alipokuwa amewatembelea kwa shughuli zake..

Shy-Rose Bhanji akiwa katika moja ya mikoa nchini Tanzania...siku zote anasema watoto wanatakiwa kufanyiwa hali ya furaha ilikuwa katika hali ya kujiamini muda wote.

Shy-Rose Bhanji akisalimiana na mmoja wa wazee moja ya mkoa wa Tanzania. Upendo kwa rika zote ikiwemo makundi maalum ya Wazee,Watoto na Wanawake ni kati ya mambo yanayofanya jamii kukubali na kuonekana kioo cha jamii.

Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi wakifurahia jambo na Shy-Rose alipokuwa amewatembelea katika shughuli za kijamii.

...Waaaacheni watoto waje kwangu,
Shy-Rose akiwa moja ya Hospitali nchini alipowatembelea Wodi ya akinamama.
Fuhara zaidi..
..Kikazi zaidi!! 
Furaha kwa kila mmoja..
Uhuru na Umoja Daima..Watoto Taifa Imara.....
..Mawio na Machweo

.......Hakika kila jambo linawezekana! "Someni sana na kwa bidii ilikuweza kutumikia Taifa" hiyo ni kauli ya Shyrose alipokuwa amewatembelea watoto wa shule ya msingi moja ya shule Nchini Tanzania.
Upendo na Ukakamavu..daima

....Popote tupo pamoja daima usiku na mchana...

....Angalau mara moja...


Shy-Rose Bhanji ni Mkuu wa Mahusiano wa Benki ya NMB nchini Tanzania, Pia ni mdau mkubwa wa maswala ya Michezo ukiwemo mchezo wa Netiboli Tanzania.
Kwa mapenzi yake binafsi kwa kuguswa na hali ya maisha ya watanzania wa rika zote, Shy-Rose ameweza kusaidia vikundi mbalimbali vya kijamii sambamba na makundi maalum kwa namna moja ama nyingine illikufanikisha Maendeleo.

Kwa nyakati tofauti, Shyrose ameweza kujumuika na makundi ya rika zote yakiwemo ya watoto na akimama katika kusaidia kwa kila hali.
Katika maswala ya Siasa, Shy-Rose ni KADA wa CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) ambapo anavyeo kadhaa ndani ya CCM, ikiwemo ya Mjumbe wa Kamati Kuu Taifa akiwakisha UVCCM.

Toa maoni yako zaidi juu ya  hili..








1 comment:

  1. Vizuri sana,jitahidi mpendwa Tunajua Mungu yupo uendeleze Taifa letu dada Shyrose.

    Picha nzuri zinakidhi ushindi uliopata.

    ReplyDelete